EventsHabari

Ibada za usiku ni mkombozi wa maisha ya wanaadamu

MHADHIRI wa Kimataifa Sheikh Fariq Naik amesema kuwa ili kuweza kuepukana na matatizo mbalimbali ya duniani ni wajibu kwa jamii ya Kiislam kurudi kwa ALLAH SW akiwa ni pamoja kufanya ibada za usiku Qiyaam al-layl

Akizungumza na waumini wa dini ya Kiislam katika msikiti wa Jamia  Zinjibar Zanzibar,Sheikh Fariq Naik  amesema kuwa miongoni mwa njia bora ya kuweza kutatua matatizo hapa duniani na kesho akhera ni kuamka kufanya ibada nyakati za usiku

Ameongeza kuwa ili kupata nguvu na umoja katika umma wa Kiislam ni wajibu kurudi katika muongozo wa Mtume Muhammad SAW

Sanjari na hilo amewataka viongozi wa familia kuwa imara kwa kuwasiamia wale wanaowaongoza kuamka kwaajili ya Qiyaam al-layl  kwani njia nzuri ya mafaniko pamoja na kuwalinda kutokana na maovu

Sheikh Fariq Naik ambae ni mtoto wa Mhadhiri wa Kimataifa Dakta Zakir Naik ameongeza kuwa swala za usiku ni sehemu nzuri kufutiwa madhambi ya mwanadamu

Mhadhiri huyo wa Kiamtaifa anatarajiwa kutoa mhadhara mwingine katika ukumbi wa Diamond Jubilee Januari 2,2025

Kongamano hilo kutoka kwa wahadhiri hao wa Kimataifa limeadaliwa na Taasisi ya The Islamic Foundation kwa ksuhirikiana na Ofisi ya Mufti Mkuu Zanzibar,huku pia likiwa limefuatiliwa na mamilioni ya waislam kupitia vyombo mbalimbali vya habari vikiwemo Radio na Tv Imaan ambavyo vilikuwa vikirusha matangazo yake moja kwa moja (LIVE)

Imehaririwa na Mrisho Salum Tozo

Related Articles

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button