Habari

Maimam chini ya taasisi ya The Islamic Foundation watakiwa kuhubiri amani

MWENYEKITI wa Taasisi ya The Islamic Foundation Aref Nahdi amewataka maimam walio chini ya Taasisi hiyo kuwa mabalozi wazuri wa kudumisha amani hasa katika kipindi hichi ambacho nchi inaeelekea katika uchaguzi mkuu

Mwenyekiti Aref amesema hayo  wakati akifungua semina ya siku mbili kwa maimamu na walimu wa dini ya Kiislam iliyoanza leo  Tarehe 25,02.2026  inayofanyikia mjini Morogoro ambapo amesema kuwa nafasi ya viongozi hao wa dini katika kudumisha amani ni kubwa

Ameongeza kuwa Taasisi hiyo itaendelea kuwa mstari wa mbele katika kufundisha mafundisho sahihi ya dini ya Kiislam ambapo yamehimiza suala la amani kwa watu wote

Awali Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya The Islamic Foundation  Sheikh Ibrahim Twaha amesema kuwa idara ya Daawa ndiyo idara yenye thamani kubwa katika taasisi hiyo hivyo kuwataka maimam hao kutokata tamaa katika kufikisha mafundisho sahihi ya dini kwa wamaumini wao

Kwa upande wao watoa mada katika Semina hiyo Sheikh Salim Bafadhili kutoka Tanga pamoja Sheikh Hassan Ahmed kutoka  Mombasa nchini Kenya wamesema kuwa mada watakazozitoa zitasaidia maimam hao kuweza kupiga hatua zaidi katika kutoa daawa

nao Baadhi ya maimam na walimu walio chini ya Taasisi ya The Islamic Foundation licha ya kuishukuru Taasisi hiyo kwa kuwaleta pamoja wamesema kuwa elimu watakayoipata itawapa mbinu zaidi za ulinganiaji wa dini ya Kiislam

Related Articles

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button